Adan Haji Yussuf ni mbunge wa Kenya. Alichaguliwa akiwa mgombea wa Economic Freedom Party katika Jimbo la Mandera West, kaunti ya Mandera, kwenye mwaka 2017.

Alihitimu shahada ya awali katika ufugaji wanyama kwenye Chuo Kikuu cha Egerton, akaendelea kusoma uzamili wa utawala, amani na usalama kwenye Africa Nazarene University. Alifanya kazi miaka mingi kwenye utumishi wa serikali, idara ya ufugaji akaendelea kufanya kazi kwa shirika za kimataifa za maendeleo kama Pact, hadi kuchaguliwa mbunge mwaka 2017.


Viungo vya Nje hariri