Aie a Mwana ni wimbo ulioandikwa na timu ya uandishi na utengenezaji ya Kifaransa-Ubelgiji inayoitwa Daniel Vangarde na Jean Kluger.

Awali ulirekodiwa mwaka 1971 chini ya jina la "Aieaoa" kwenye albamu ya Le Monde fabuleux des Yamasuki. Mwaka 1975, toleo lenye mashairi kwa kiasi kikubwa ya Kiswahili lilirekodiwa na kundi la Kiafrika linalotayarisha muziki nchini Ubelgiji, Black Blood, na kutolewa kama "A.I.E. (A Mwana)". Toleo hili la Kiswahili pia lilijitokeza katika mchezo wa video wa mpira wa miguu, Pro Evolution Soccer 2011.

Mwaka 1981, "Aie a Mwana" ulikuwa wimbo wa kwanza kutolewa na kundi la Kiingereza, Bananarama.

Mwaka 2010, ukionyesha melody ile ile lakini mashairi mapya na ukitoa kama "Helele", ulikuwa wimbo rasmi wa Kombe la Dunia la FIFA mwaka 2010, katika toleo lililotumbuizwa na Velile na Safri Duo.

Marejeo hariri