Apolonia (Makedonia)

Apolonia (kwa Kigiriki: Ἀπολλωνία, Apollonia) ulikuwa mji wa Ugiriki kaskazini mashariki[1][2], karibu na Nea Apollonia ya leo.

Apollonia (Mygdonia) ulikuwa upande wa kaskazini, na ni tofauti na Apollonia (Chalcidice) uliokuwa kusini.

Unatajwa na Biblia ya Kikristo kwa kuwa mwaka 49 au 50 Mtume Paulo, katika safari yake ya pili ya kimisionari, alipitia huko baada ya kukimbia Filipi kutokana na dhuluma akielekea Thesalonike pamoja na Sila (Mdo 17:1).

Tanbihi hariri

  1. Athen. viii. p. 334, e.
  2. Antonine Itinerary pp. 320, 330; Itin. Hierosol. p. 605; Tabula Peutingeriana
  Makala hii kuhusu maeneo ya Ugiriki bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Apolonia (Makedonia) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.