Bambata ni mradi wa muziki wa Afrika Kusini iliyozalisha albamu tatu maarufu 1906 mwaka 2000, ukhandampondo (kodi ya Kichwa) mwaka 2002, na Abashokobezi 19062006 mwaka 2006. Nguvu kubwa ya mradi huu umewekezwa na Sipho Sithole, mkurugenzi na mwanzilishi wa Native Rhythms Productions, Philangezwi Bongani Nkwanyana, Mathufela Zuma na Bheki Khoza. Walichagua jina Bambata kwa lengo la kumuenzi Bambatha kaMancinza chifu wa kabila la amaZondi katika koloni ya Natal (Kwa sasa ni Kwa Zulu-Natal) aliyekuwa na uhusika mkubwa katika uasi wa Bambatha kuwapinga waingereza mwaka 1906 plae ambapo kodi ya kichwa ilipoongezwa kutoka kodi kwa kaya na kuwa kodi kwa kichwa.

Bhambatha akiwa na msaidizi wake aliye simama upande wa kulia

Tuzo na Teuzi hariri

Albamu ya kwanza ya Bambata 1906 iliteuliwa katika jamii tatu katika tuzo za muziki ya Afrika ya Kusini 2001 kama chipukizi bora, muziki bora wa Zulu na Muziki bora wa kisasa ya watu wazima.Sipho Sithole pia aliteuliwa kama mtayarishaji bora.[1]

Mwaka Sherehe ya Tuzo Tuzo Kazi/Mpokeaji Matokeo
2001 Tuzo ya 7 ya muziki wa Afrika Kusini Chipukizi bora 1906 Aliteuliwa
Muziki bora wa Zulu 1906 Aliteuliwa
Albamu bora ya kisasa ya Watu wazima: Ya Kiafrika 1906 Aliteuliwa

Diskografia hariri

  • 2000: 1906
  • 2002: ukhandampondo (Kodi ya Kichwa)
  • 2006: Abashokobezi 1906–2006

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Bambata kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.