"Chaguo Langu" ni jina la filamu iliyotoka 2012 kutoka nchini Tanzania. Ndani yake anakuja Jacqueline Wolper, Single Mtambalike na Adam Kuambiana. Filamu imeongozwa na Mtambalike na kutayarishwa na Bulls Entertainment. Filamu inaelezea hadithi ya binti aliyelelewa katika mazingira ya dini kupita kiasi, lakini anakutana na changamoto ya kufuata tabia zisizo za kimaadili hasa mumewe kutaka avae mavazi yasiyoendana na maadili aliyokuziwa nayo. Baadaye anapata vishawishi kadhaa kutoka kwa mganga wa kienyeji na kumpoteza mumewe katika mazingira ya kichawi.[1]

Chaguo Langu

Posta ya Chaguo Langu
Imeongozwa na Single Mtambalike
Imetayarishwa na Bulls Entertainment
Imetungwa na Single Mtambalike
Nyota Jacqueline Wolper
Single Mtambalike
Adam Kuambiana
Sinematografi Kabuti Onyango
Imesambazwa na Steps Entertainment
Imetolewa tar. 2012
Nchi Tanzania
Lugha Kiswahili

Viungo vya Nje hariri


Marejeo hariri

  1. Chaguo Langu Archived 9 Januari 2017 at the Wayback Machine. katika Bongo Cinema.
  Makala hii kuhusu filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chaguo Langu kama waigizaji wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.