Chama cha Skauti Sierra Leone

Shirika

Chama cha skauti cha Sierra Leone ni shirikisho la skauti la Sierra Leone lililoanzishwa mano mwaka 1909 na kuwa mwanachama wa Shirika la Harakati za Skauti Duniani mnamo mwaka 1964, hadi kufikia mwaka 2011 shirikisho hili lilikuwa na jumla ya wanachama 11,749 [1]

Chama cha Skauti Sierra Leone

Mnamo mwaka 1971, Emile F. Luke alipewa Mbwa wa Shaba, heshima pekee ya Shirikisho la Harakati za Skauti Duniani, inayotolewa na Kamati ya Skauti ya Dunia kwa huduma bora kwa Skauti wa dunia.

Chama cha Skauti cha Sierra Leone kilikuwa mwenyeji wa Mkutano wa Tatu wa Kanda ya Magharibi mwa Afrika na Kambi ya Vijana. Skauti 75 walishiriki kutoka nchi 9 za Magharibi mwa Afrika.

Mgogoro wa kijeshi wa hivi karibuni umepunguza shughuli na mawasiliano ya Skauti. Tangu wakati huo, Skauti wamepambana kuendelea na uanachama wake na shughuli hadi mwaka 2014, walipolazimika kubadilisha jina ili kuanza awamu mpya. Tangu wakati huo, wameandaa mfululizo wa ushirikiano, mafunzo, na uajiri ili kutekeleza huduma zake za kawaida.[1]


Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 Triennal review: Census as at 1 December 2010. World Organization of the Scout Movement. Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-05-08. Iliwekwa mnamo 2011-01-13.