Chama cha kikomunisti

Chama cha kikomunisti ni chama cha kisiasa kinacholenga kufikisha jamii katika hali ya ukomunisti yaani jamii bila matabaka ya matajiri na maskini na bila watu wenye mali nyingi kuliko wengine. Katika nadharia hali hii ya ukomunisti imedhaniwa kuwa bila utawala wa watu juu ya wengine lakini nadharia hii inadai pia ya kwamba kuna kipindi cha mpito ambako chama cha kikomunisti kinatawala kwa namna ya kidikteta hadi mabaki ya utaratibu wa kale yamekwisha ambayo yanaweza kuzuia au kuchelewesha maendeleo ya kuelekea ukomunisti.

Nyundo na Mundu, ni alama ya ukomunisti na sehemu ya nembo ya vyama vya kikomunisti

Vyama vya Wakomunisti vilifaulu kushika serikali katika Urusi tangu 1917, katika Umoja wa Kisovyeti tangu mnamo 1920 / 1924 halafu katika nchi za Ulaya ya Mashariki tangu 1945 / 46. Katika China, Korea ya Kaskazini na Vietnam ya Kaskazini Wakomunisti walitawala tangu mnamo 1948 /49. Vyama mbalimbali katika nchi kadhaa za Afrika vilifuata mtindo wa Wakomunisti kwa namna fulani na kushika utawala kwa miaka kadhaa.

Utawala wa vyama vya kikomunisti uliporomoka mnamo 1989 katika nchi nyingi na leo hii (2011) vyama vya kikomunisti vinatawala katika nchi chache pekee kama vile China, Vietnam na Kuba. Lakini havilengi tena kufikia shabaha ya ukomunisti.