Emirates Palace (Kiarabu: قصر الإمارات) ni hoteli ya starehe iliyopo mjini Abu Dhabi, UAE.

Emirates Palace
Mazingira ya ndani ya Emirates Palace

Ujenzi hariri

Ilifunguliwa mwezi Novemba 2005 lakini baadhi ya mikahawa na maduka hayakuwa wazi hadi 2006. Hoteli ilijengwa na inamilikiwa na serikali ya Abu Dhabi, na kwa sasa inasimamiwa na Kempinski Group.

Gharama ya kujenga hoteli hii ilikuwa dola bilioni 3. Emirates Palace ina upana wa 850,000 m². Kuna nafasi ya kuweka magari 2,500. Kuna mabwawa mawili ya kuogelea. Hoteli hii ina marina yake pamoja na kituo cha kushusha helikopta. Kulingana na gazeti la New York Times, Emirates Palace ni hoteli ya ghali zaidi kuwahi kujengwa [1]

Vipengele hariri

Nje hariri

Hoteli ina miviringo kama ya mskiti takriban 114 iliyo na urefu wa mita 60.

Ndani hariri

Vyumba vingi vimemaalizwa kwa dhahabu na marumaru. Eneo kuu la hoteli hii ina ukumbi wa marumaru pamoja na dhahabu. Ghorofa ya juu kabisa ina vyumba sita viavyotumiwa na maafisa au watawala muhimu wanaotembelea UAE. [1][2] Hoteli pia ina ukumbi mkubwa wa mkutano.

Vyumba na bei zake hariri

Kwa jumla, hoteli ina vyumba 302 na vyumba vya waheshimiwa 92. Vilevile, hoteli hii ina vyumba vingine 16 kwenye ghorofa ya sita na saba. Vyumba 22 vimetengewa wakuu wa nchi na wageni wao. Gharama ya kulala huanzia $400 kwa usiku mmoja kwenye Coral Room; na The Palace Grand Suite ni ghali zaidi - $11,500 per usiku. [3]

Viungo vya Nje hariri

Marejeo hariri

  1. "Emirates Palace". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-10-30. Iliwekwa mnamo 2010-01-05. 
  2. "Emirates Palace". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2007-10-30. Iliwekwa mnamo 2010-01-05. 
  3. "Emirates Palace Hotel". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2009-12-31. Iliwekwa mnamo 2010-01-05.