Ernest Bai Koroma (alizaliwa Makeni, wilaya ya Bombali, kaskazini mwa Sierra Leone, 2 Oktoba 1953) alikuwa rais wa Sierra Leone tangu 17 Septemba 2007.

Ernest Bai Koroma

Koroma alikuwa mwanabiashara hadi kujiunga na siasa mwaka 2002 alipokuwa mgombea wa urais wa chama cha All People's Congress dhidi ya rais Ahmad Tejan Kabbah. Aliposhindwa akaongoza upinzani bungeni. Katika uchaguzi uliofuata wa mwaka 2007 alimaliza kama mgombea mwenye kura nyingi. Hakufikia nusu za kura hivyo akasimama tena katika awamu ya pili ya uchaguzi akashinda akaapishwa tarehe 17 Septemba kuwa rais mpya.

Mnamo Desemba 2023, Ernest Bay Koroma aliwekwa chini ya kizuizi cha nyumbani baada ya siku mbili za kuhojiwa kufuatia matukio yaliyotokea Novemba 26, 2023 wakati wa maandamano, yaliyofafanuliwa kama jaribio la mapinduzi ya serikali na mamlaka ya Sierra Leone.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ernest Bai Koroma kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.