Fat'ha ni sura ya mwanzo kabisa (sura namba moja) katika mtiririko wa sura zilizomo katika Qur'an Tukufu. Ni sura ambayo inaaminika kuwa miongoni mwa dua kubwa kabisa katika Qur'an, hivi kwamba katika kila ibada (Swala) ya Mwislamu yeyote lazima aitangulize sura hiyo kabla ya sura nyingine yoyote.