Flotufolastati F-18

Flotufolastati F-18 (Flotufolastat F-18), inayouzwa kwa jina la chapa Posluma, ni wakala wa uchunguzi jumla ya damu na kiasi cha plasma inayotumika katika tomografia ya utoaji wa positron ya saratani ya kibofu.[1] Hutumika hasa katika ugonjwa chanya wa antijeni maalumu ya utando wa kibofu ili kutafuta kuenea au kujirudia kwake.[1] Inatolewa kwa njia ya kudungwa sindano kwenye mshipa.[1]

Madhara yake ya kawaida ni pamoja na kuhara, shinikizo la damu, na maumivu kwenye eneo la sindano.[1] Madhara yake mengine ni pamoja na kupatwa na mnururisho.[1] Dutu inayofanya kazi katika dawa hii ni galiumu (gallium) ya flotufolastat F-18.[1]

Flotufolastati F-18 iliidhinishwa kwa ajili ya matumizi ya kimatibabu nchini Marekani mwaka wa 2023.[1]

Marejeo

hariri
  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 1.4 1.5 1.6 "Posluma- flotufolastat f-18 injection". DailyMed. 2 Juni 2023. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 26 Juni 2023. Iliwekwa mnamo 25 Juni 2023.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Flotufolastati F-18 kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.