Glakoma

(Elekezwa kutoka Glaucoma)

Glakoma (kwa Kiingereza: glaucoma) ni ugonjwa unaosababishwa na uharibifu wa jicho.

Macho ya mtu mwenye glakoma.

Ugonjwa huu husababishwa na shinikizo linaloongezeka katika jicho. Shinikizo hilo husababisha uharibifu wa mishipa ya optic (optic nerves) katika jicho. Hii inaweza kusababisha upofu na maumivu makali katika jicho.

Wakati mwingine ni vigumu kwa watu kugundua kuwa wana glakoma, maono yanapotea polepole sana. Maono yakipotea kwa sababu ya glakoma haiwezekani kurudishwa hata kwa kutumia miwani ya lenzi yoyote.

Kuna aina mbili za glakoma, aina ambayo hutokea haraka sana, na aina ambayo hutokea polepole na kwa muda mrefu. Glakoma ndiyo sababu ya pili ya upofu ulimwenguni. Mara nyingi glakoma ni ugonjwa wa kurithi kutoka kwa wazazi.

Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Glakoma kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.