Kisegeju ni lugha ya Kibantu nchini Tanzania inayozungumzwa na Wasegeju. Idadi ya Wasegeju imehesabiwa kuwa watu 15,000 lakini ni watu 7000 tu ambao bado wanajua kuongea Kisegeju, Wasegeju wengi wakitumia lugha za Kiswahili na Kidigo badala ya lugha yao. Kwa hiyo lugha imeanza kutoweka. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kisegeju iko katika kundi la E70. Wengine wanasema kuwa ni sawa na Kidhaiso.

Viungo vya nje hariri

Marejeo hariri

  • Maho, Jouni & Bonny Sands. 2002. The languages of Tanzania: a bibliography. (Orientalia et africana gothoburgensia, no 17.) Göteborg: Acta Universitatis Gothoburgensis. Pp ix, 428. ISBN 91-7346-454-6

Kitabu hiki kinataja marejeo mengine kama:

  • Nurse, Derek. 1982. Segeju and Daisu: a case study of evidence from oral tradition and comparative linguistics. History in Africa, 9, uk.175-208.
  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kisegeju kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.