Kutubu : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Mstari 30:
Kutubu ni nyota pache yenye sehemu tatu : nyota kuu inayojulikana kama α Umi Aa (au A<sup>1</sup>) inayozungukwa na msindikaji mdogo α Umi Ab (au A<sup>2</sup>) na hizi mbili zinazungukana na nyota ya tatu α Umi B kitovu cha graviti cha pamoja.
 
Kutubu ilitambuliwa kwenye mwaka 1780 na [[William Herschel]] kwa darubini kuwa [[nyota pacha]] yaani mfumo wa nyota mbili za α Umi A na α Umi B. Wakati ule [[darubini]] ya Herschel ilikuwa kati ya vifaa bora duniani. Kwa kutumia [[Darubini ya Angani ya Hubble]] ilitambuliwa kwenye mwaka 2006 ya kwamba pia nyota ya A yenyewe ni nyota pacha na sasa Polaris yote inajulikana kama mfumo wa nyota tatu zinazoitwa α Umi A<sup>1</sup>, α Umi A<sup>2</sup> na α Umi B.
Nyota kuu ni Kutubu A<sup>1</sup> (Polaris Aa) ambayo ni [[nyota geugeu]] yenye masi ya Jua mara 5 iking’ara mara 1200 kuliko Jua letu. Kutokana na mng’aro mkubwa inapangwa katika kundi la [[nyota jitu kuu]] . Mwangaza wa α Umi Aa ulibadilikabadilika kati ya mag 1.86 hadi 2.13 wakati wa kurekodiwa kama miaka 100 iliyopita. Baadaye kiwango hiki kilipungua kwa muda mrefu lakini kwa miaka ya nyuma kimeanza kuongezeka tena<ref>Lee & alii (2008)</ref>