Chansela (kiongozi) : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
No edit summary
(Hakuna tofauti)

Pitio la 08:40, 12 Juni 2006

Chansella (Kijerumani: "Kanzler") ni cheo cha mkuu wa serikali, lakini si mkuu wa dola, katika Ujerumani na Austria. Hapa inafanana na cheo cha waziri mkuu.

Menginevyo neno hili limemaanisha vyeo mbalimbali vya nagzi tofauti. Asili ya neno ni Kilatini "cancellarius" la kumtaja mtu mwenye ofisi aliyewajibika kutoa vyeti rasmi. Wakati mwingine neno lilimtaja mwandishi tu. Lakini lilitumika pia kwa ajili ya cheo cha "Mwandishi Mkuu" kilichoweza kufanana na "Katibu Mkuu" kwa Kiswahili yaani msimamizi wa kazi ya utawala.

Katika nchi zenye lugha ya Kijerumani cheo kikawa cheo cha mkuu wa serikali. Uswisi linamaanisha Katibu Mkuu wa ofisi ya serikali.

Huko Uingereza chansella ("Chancellor") ni cheo cha waziri ya fedha.

Cheo cha chansella kinapatikana kimataifa pia katika vyuo vikuu vya nchi mbalimbali likimtaja ama mkuu wa chuo au mkuu wa utawala wa chuo.