'''Kilima''' ni mwinuko wa ardhi ambao uko juu kuliko eneo linalokizungukalinalouzunguka lakini ni ndogomdogo kuliko ule wa [[mlima]]. Vilima ni miinuko ya chini zaidi kuliko milima. Kwa [[lugha]] nyingine ni mlima mdogo, kama [[Kiswahili]] kinavyoonyesha wazi. Uso wa kilima ni imara zaidi kuliko ile ya [[tuta la mchanga]].
Hakuna [[ufafanuzi]] kamili unaokubaliwa kote kuhusu tofauti kati ya kilima na mlima unaokubaliwa kote. Katika sehemu za [[tambarare]] mwinuko wa [[mita]] [[mia]] kadhaa unaweza kuitwa "mlima", kinyume chake katika sehemu za milima mirefu mwinuko wa mita 1000 unaweza kuitwa "kilima",. Kwa mfano, miinuko ya Ngong karibu na [[Nairobi]] huitwa "[[Ngong Hills]]" ingawa inafikia [[kimo]] cha zaidi ya mita 2,000 juu ya [[usawa wa bahari]]. Kwa jumla kilima hutazamiwahutazamwa kuwa kidogo na bila mtelemko mkali kama mlima kamili.
[[Asili]] ya vilima mara nyingi ni sawa na asili ya milima; kunjamano ya [[ganda la Dunia]] au vilima kama mabaki ya miinuko mikubwamirefu zaidi, kwa mfano kutokana na [[mmomonyoko]] wa milima mikubwa.