Songea (mji) : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
|||
Mstari 1:
'''Songea''' ni mji nchini [[Tanzania]] ambao ni makao makuu ya [[Mkoa wa Ruvuma]]. Kulingana na sensa ya mwaka 2002 idadi ya wakazi wake ilihesabiwa kuwa 131,336 [http://www.tanzania.go.tz/census/districts/songeaurban.htm].
Kuna barabara ya lami kutoka Songea kupitia [[Njombe]] hadi barabara kuu ya [[Dar es Salaam]] - [[Mbeya]]. Barabara ya kwenda pwani kupitia [[Tunduru]] na [[Masasi]] ni mbaya mara nyingi haipitiki wakati wa mvua.
==Jiografia==
Mji uko kwenye kimo cha [[m]] 1210 [[juu ya UB]] katika nchi ya [[Ungoni]] kwenye [[nyanda za juu za kusini za Tanzania]]. Chanzo cha [[mto Ruvuma]] kipo karibu na mji.
==Historia==
Jina la Songea ni kumbukumbu ya chifu Songea wa [[Wangoni]] aliyekuwa na ikulu yake hapa wakati wa kuenea kwa [[Afrika ya Mashariki ya Kijerumani|ukoloni wa Ujerumani]] akauawa na Wajerumani wa kati wa [[vita ya majimaji]].
Mji wa Songea (iliyoandikwa Ssongea wakati ule) ulianzishwa mwaka [[1897]] kama kituo cha kijeshi cha Kijerumani. Ukakua kuwa makao makuu ya utawala wa mkoa Songea wa [[Afrika ya Mashariki ya Kijerumani]].
Mazingira ya mji yaliathiriwa vibaya na vita ya majimaji na ukandamizaji wake na Wajerumani.
Songea ikaendelea kuwa makao makuu ya mkoa wakati wa uatwala wa Uingereza katika [[Tanganyika]] na baada ya uhuru katika Tanzania huria.
{{mbegu}}
|