'''Wikipedia''' ni [[kamusi elezo]] huru ya [[lugha]] nyingi katika [[mtandao]] wa [[wavuti]].
Inatumia taratibu za [[wikiwiki]]. Ni bure kabisa, na inaweza kusomwa, kuandikwa, na kuhaririwa na [[mtu]] yeyote, popote pale. Yaani kila mtu anaweza kuchangia [[makala]] akiwa na [[uhuru]] wa kuboresha makala zilizopo kwa kuzihariri.
[[Kamusi]] hii inajengwa kwa utaratibu huria ambao umejengwa juu ya [[falsafa]] ya [[ushirikiano]] inayokuwa kwa kasi.
Falsafa hii inaonekana katika vuguvugu la [[programu huria ya tarakilishi]], [[mikutano huria]], [[demokrasia huria]], n.k.
Wikipedia inaweza kusomwa pia nje ya mtandao kwa kutumia [[programu huria]] ya [[Kiwix]].