Tengamaji : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika 'thumb|300px|Ramani ya beseni kubwa kwenye bara la Afrika ''(tahajia ya Kijerumani)'' '''Te...' |
N |
||
Mstari 1:
[[Picha:EN Bazinul hidrografic al Raului Latorita, Romania.jpg|thumb|300px|Beseni ya mto Lotro, Romania; mstari mwekundu ni tengamaji]]
[[Picha:Karte der Einzugsgebiete der großen Gewässer Afrikas.png|thumb|300px|Ramani ya beseni kubwa kwenye bara la Afrika ''(tahajia ya Kijerumani)'']]
'''Tengamaji''' ([[ing.]] ''drainage divide''<ref>Kwa lugha ya Kiingereza kuna majina yanayotofautiana katika Kiingereza cha Britania na Marekani, kama vile: water divide, divide, ridgeline, watershed, water parting</ref>) ni sehemu za juu zinazotenganisha [[beseni]] za [[mito]] inayokusanya maji ya eneo fulani.
Kwa lugha nyingine tengamaji ni sehemu ambako matone mawili ya mvua yanayoanguka mahali pa karibu yatatiririka mtelemko kuelekea mito tofauti.
Tengamaji mara nyingi ni safu ya milima au vilima kwa mfano ni safu za [[Uporoto]] na [[Kipengere]] katika Tanzania Kusini zinatotenganisha maji kati ya beseni za [[Ruaha Mkuu]] na [[Mto Zambezi]] (kupitia [[Ziwa Nyasa]]). Tengamaji katika tambarare haitambuliki kirahisi hivi.
Katika elimu ya [[hidrolojia]] wataalamu hutofautisha ngazi mbalimbali
*'''tengamaji kuu''' au tengamaji ya kibara: mstari unaopita katika bara na kusababisha mvua kuelekea bahari tofauti; kwa mfano tengamaji kuu ya [[Amerika Kaskazini]] inafuata safu ya [[Rocky Mountains]] na kugawa bara lote kati ya beseni kuu za Atlantiki na Pasifiki. Ndani ya beseni hizi kuu kuna tena beseni za mito tofauti inayofikisha maji baharini.
Barani Afrika tengamaji ya kibara muhimu ni tengamaji ya Kongo na Naili.
*'''tengamaji kubwa''' ni mstari kati ya beseni za mito zinazokusanya maji ya eneo ka kuyafikisha katika bahari ileile; kwa mfano nchini Tanzania tengamaji kati ya Ruaha Kuu na Zambezi kwa sababu mito yote miwili inaishia katika Bahari Hindi. Nchini kenya mfano ni milima ya Aberdare ambayo ni tengamaji kati ya beseni za mto Athi na mto Tana inayoishia yote katika Bahari Hindi.
* '''tengamaji ya kawaida''' ni mstari kati ya beseni mbili zitakazoungana baadaye, mfano tengamaji kati ya beseni ya Missouri na Missisippi ya juu. Mfano nchini Tanzania ni tengamaji kati ya beseni za [[Ruaha Mkuu]] na [[Mto Kilombero]] inayokutana baadaye kwenye [[Rufiji]].
==Marejeo==
{{references}}
[[jamii:Jiografia]]
|