VIPENGELE VYA FASIHI SIMULIZI : Tofauti kati ya masahihisho

Content deleted Content added
Ukurasa ulianzishwa kwa kuandika 'Fasihi ndiyo aina pekee ya sanaa inayotumia lugha kujitambulisha au kujitofautisha na aina nyingine za sanaa. fasihi zipo za aina mbili,nazo ni 1*Fasihi simuli....'
(Hakuna tofauti)

Pitio la 13:06, 8 Oktoba 2016

Fasihi ndiyo aina pekee ya sanaa inayotumia lugha kujitambulisha au kujitofautisha na aina nyingine za sanaa. fasihi zipo za aina mbili,nazo ni 1*Fasihi simuli. 2*Fasihi andishi.

  FASIHI SIMULIZI

Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mazungumzo ya mdomo ili kufikisha ujumbe kwa hadhira.Aina hii ya fasihi ndiyo iliyokuwapo tangu zamani kabisa mwanadamu alipoanza kuishi yaani ilianza pale mwanadamu alipochangamana na wenzake katika kufanya mambo mbalimbali mfano,shughuli za biashara,kilimo,na nyinginezo.

   AINA ZA FASIHI SIMULIZI

Utanzu huu wa fasihi una vipera au aina kuu nne,nazo ni 1*Hadithi. 2*Ushairi. 3*Semi. 4*maigizo.

   SEMI

Semi ni tungo fupi za kisanaa zitumiazo picha na tamathali kuelezea maudhui yanayobeba mafunzo ya kijamii.

   TANZU ZA SEMI

Semi ina vipera au tanzu sita ambazo ni, 1*Methali 2*Vitendawili 3*Nahau 4*Misemo 5*Mafumbo 6*Mizungu

    METHALI

Methali ni semi fupi zenye mpangilio maalumu wa maneno ambazo huelezea kwa muhtasari mafumbo na mawazo mazito yanayotokana na uzoefu wa kijamii. Methali huundwa na vipande viwili vya maneno vyenye fikra yurani.Kipande cha kwanza huashilia tendo au sharti na kipannde cha pili huashilia matokeo ya tendo au sharti hilo. Mfano wa methali 1*Mcheka kilema,hali hakija mfika. 2*Kupotea njia, ndiko kujua njia. 3*Mchelea mwana kulia, utalia wewe. Maana ya methali hutegenea muktadha au wakati maalumu kati jamii.

  KAZI ZA METHALI

Methali zina kazi nyingi katika jamii yoyote ile kama vile, 1*Kuionya jamii inayohusika au inayopewa methali hiyo. 2*Kuishauri jamii inayopewa au kutamkiwa methali hiyo. 3*Kuihiza jamii inayohusika. 4*Kukejeli mambio mbalimbali yanayofanyika ndani ya jamii husika.