Iwiji : Tofauti kati ya masahihisho
Content deleted Content added
No edit summary |
Tags: Mobile edit Mobile web edit |
||
Mstari 23:
==Kijiji cha Izyira==
Kijiji cha Izyira
Misitu hii ni muhimu kwa kuwa ndicho chanzo kikuu cha mito mikuu mitatu ambayo ni Mto Magole, Mto Salaga na Mto Mafumbo. Mito hii ndio chanzo pekee ambayo
Izyira hukaliwa na makabila matatu ya [[Wanyiha]], [[Wandali]] na [[Wamalila]]. Kijiji hiki kuna mila na desturi zake kikiongozwa na mila za kijadi. Kiongozi akiitwa mwene wa ukoo wa Mwazembe. Kati ya Wakristo kuna hasa madhehebu yaliyo kwenye jumuiya ya CCT. Kijiji hiki kina shule tatu. Izyira ni shule mama iliyoanzaishwa mnamo miaka ya 1957 kwa mfumo wa shule za TAPA iliyoanza na mwalimu mzawa Winfred Mtindo Mwazembe baadaye zilianzishwa shule mbili kutokana na ongezeko la watu ambazo ni Mwenge na shule ya msingi Masewe. Pia wananchi katika mfumo wa kila kata kujenga shule ya sekondari kijiji kama kijiji walijenga shule ya sekondari ya kijiji kwa mpango wa kijitolea pamoja na kuwa na shule ya sekondari ya kata ambayo ipo makao ya kata pale Iwiji pia mwaka 2009 shule ya sekondari ilifunguliwa katika kijiji cha Izyira mwezi April 29 chini ya mkuu wa shule Godlove Ngonde
Kijiji hiki kinahudumiwa na barabara kuu kutoka mbalizi ikipitia vijiji vifuatavyo mbalizi Izumbwe I, Mganjo, Isangati Santilya, Shipongo, Ilembo, Italazya, Shigamba, Izumbwe II. Iwiji barabara inagawanyika, kushoto inakwenda makao makuu ya Wilaya ya Ileje yaani Itumba na kulia barabara hii ndiyo inakwenda moja kwa moja Izyira hatimaye huendelea Wilaya ya Mbozi kupitia vijiji vya Hezya, ,Nyimbili, Ilengo, Shumba, Hasamba na kuungana tena na barabara kuu ya Dar es Salaam mpaka Zambia pale makao mkuu ya Wilaya ya Vwawa.
Chakula chao kikuu kinatokana na mazao yaani mahindi, ndizi na viazi vitamu. Zao la biashara ni kahawa. Mito mitatu hupitia kijiji hiki, mto Magole upo mashariki sambamba na kijito kidogo kiitwacho Itaga katikati kuna kijito kingine Salaga magharibi kuna mto mkubwa Mafumbo na magharibi kuna kijito kingine shongo . Mito yote hii ndio chanzo kikuu cha uzalishaji wa chakula cha
Kutokana na ongezeko la watu misitu hii miaka ya karibuni kumekuwa na uharibifu mkubwa na kusababisha mito hii kupungua sana tena sana kwa ujazo wa maji na kusababisha kupungua kwa kiwango cha unyeshaji wa mvua, kama hatutakuwa na mkakati wa kuzuia uharibifu huu wa misitu hii msitu
Kijiji hiki, pamoja na kuwa na vitongoji kumi vinahudumiwa na zahanati moja tu.
Kata ya Izyira ina Jumla ya vijiji vinne ambavyo ni Izyira, Masewe, Inuka na Mapita ikiwa ni kijiji kilichotokea baada ya kugawa kijiji cha Izyira
==Marejeo==
{{marejeo}}
|