Malai
Malai (pia krimu kutoka Kiingereza: cream), ni mafuta yanayopatikana kiasili katika maziwa ya wanyama. Baada ya kukamua maziwa, malai hukusanyika kwenye uso wa maziwa kama utandu. Utandu huo hutolewa na kukusanywa.
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/ec/Milk_heavy_cream_B.jpg/220px-Milk_heavy_cream_B.jpg)
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/16/Cr%C3%A8me_Chantilly.jpg/220px-Cr%C3%A8me_Chantilly.jpg)
Malai hutumiwa kutengeneza samli, siagi na jibini. Pia katika upishi na kutengeneza vyakula mbalimbali kama aisikrimu.