Mamochisane (fl. 1851) alikuwa Mfalme wa Makololo ambaye alitawala juu ya watu wengi, lakini hasa Watu wa Lozi katika eneo la Barotse, ambayo kwa sasa ni Magharibi mwa Zambia, mwaka 1851. Baadaye alikuwa mke wa Mfalme Sipopa Lutangu.

Maisha hariri

Mamochisane alikuwa binti wa Mfalme Sebetwane, dada wa kambo wa Mwanamfalme Sekeletu na dada au dada wa kambo wa Mwanamfalme Mpepe. Alikuwa mpwa wa mfalme Mbololo.

Alichukua uongozi baada ya kifo cha baba yake mnamo mwaka 1851, kama alivyokusudia muda mrefu kabla ya kifo chake, hata kama alikuwa na ndugu wa kiume. Aliendeleza urafiki na msafiri David Livingstone, ambao ulianzishwa na baba yake, akimpa ruhusa ya kutembelea ufalme wake wote.

Livingstone aliporudi mwaka 1853 kwenye mji mkuu wa Makololo, Linyati, aligundua kwamba muda mfupi baada ya kifo cha baba yake alijiuzulu kwa niaba ya kaka yake Sekeletu, ambaye alikuwa mfalme mpya. Kulingana na maelezo ya Livingstone, sababu ilikuwa ni kutaka kuwa na mume thabiti na familia iliyomilikiwa nae, wakati akiwa kiongozi alilazimika kuolewa na wanaume wengi kwa hiyo hakuna yeyote atakaepata mamlaka mengi sana.

Mamochisane alikuwa na mpwa aliyeitwa Litali; alikuwa mtoto wa Sekeletu. Alifunga ndoa na Sipopa Lutangu.

Fasihi hariri

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mamochisane kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.