Mbinu

ukarasa wa maana wa Wikimedia

Mbinu ni hatua zinazofuatwa ili kufanya hadi kukamilisha kazi, jukumu au tendo fulani.

Ubunifu, yaani uwezo wa kubuni, umestawi sana katika binadamu na kumfanya asichoke kutafuta majibu mapya kwa maswali yanayomkera, na njia mpya za kutatua matatizo yake.

Pamoja na hayo, baadhi ya watu wana sifa ya pekee katika uwezo huo hata wakachangia zaidi maendeleo, k.mf. ya teknolojia.

Kwa kawaida mbinu iliyothibitisha ufanisi wake inaigwa na watu wengine.

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mbinu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.