Mdudu-koleo
Mdudu-koleo (Anisolabis maritima)
Mdudu-koleo (Anisolabis maritima)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Arthropoda (Wanyama wenye mwili wa pingili na miguu ya kuunga wasio na ugwe wa mgongo kama wadudu, nge, buibui)
Nusufaila: Hexapoda (Arithropodi wenye miguu sita)
(bila tabaka): Dicondylia (Wadudu walio na mandibula zenye condyle mbili)
Ngeli: Insecta (Wadudu)
Linnaeus, 1758
Nusungeli: Pterygota (Wadudu wenye mabawa)
Lang, 1888
Oda: Dermaptera
De Geer, 1773
Ngazi za chini

Nusuoda 4:

Wadudu-koleo ni wadudu wadogo wa oda Dermaptera (derma = ngozi, ptera = mabawa) ambao wana serki kwa umbo wa koleo. Serki hizi hutumika kwa kushika mawindo, kwa kujitetea, kwa kukunja mabawa ya nyuma na wakati wa kujamiiana. Mabawa ya nyuma yakunjwa ili kufichwa chini ya yale ya mbele yaliyo mafupi.

Kuna spishi zinazoishi juu ya wanyama, lakini takriban spishi zote huishi nje na hula kila aina ya chakula: majani, maua, wadudu wadogo, maada ya mimea na wanyama waliokufa. Spishi kadhaa, kama mdudu-koleo wa Ulaya, zinaweza kuwa wasumbufu na kusababisha hasara katika mashamba. Lakini spishi nyingi zinasaidia wakulima kwa sababu wanakula wadudu wengine wasumbufu, kama vidukari.

Spishi kadhaa za Afrika ya Mashariki hariri

  • Anisolabis felix
  • Anisolabis jeanneli
  • Anisolabis maritima
  • Dihybocercus confusus
  • Isolabis bicolor
  • Isolabis braueri
  • Iolabis proxima
  • Isolabis rufa
  • Isolabis transversa
  • Isolabis unicolor
  • Isolabis usambarana

Picha hariri

  Makala hii kuhusu mdudu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mdudu-koleo kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  Makala hiyo kuhusu "Mdudu-koleo" inatumia jina ambalo halijakuwepo kwa lugha ya Kiswahili. Jina hili linapendekezwa kwa jina la mnyama huyu au wanyama hawa amba(ye)(o) ha(wa)na jina kwa sasa.

Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao kwenye ukurasa wa majadiliano ya makala.
Kamusi za Kiswahili hazina jina kwa mnyama huyu au wanyama hawa.