Millicent Dolly May Small (6 Oktoba 1947 – 5 Mei 2020),[1][2] alikuwa mwimbaji wa Jamaika anayejulikana zaidi kwa kibao chake cha kimataifa My Boy Lollipop cha mwaka 1964. Wimbo huo ulifikia namba mbili kwenye chati za UK Singles Chart na Billboard Hot 100, na kuuza zaidi ya nakala milioni saba duniani kote. Pia ilikuwa nyimbo iliyo tamba zaidi katika lebo ya Island na ulisaidia lebo hiyo kufikia mafanikio makubwa. Alikuwa nyota wa kwanza wa kimataifa wa kurekodi kutoka Karibiani na msanii wa kike aliyefanikiwa zaidi kutoka eneo hilo.[3][4]

Small akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Schiphol Amsterdam kutoka Jamaika mwaka 1964

Marejeo

hariri
  1. Chris Salewicz. "Millie Small obituary". 
  2. Bruce Eder. "Millie Small | Biography". AllMusic. Iliwekwa mnamo 27 Januari 2014.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Laurence Cane-Honeysett, "Millie Small, the Lollipop Girl", Record Collector. Retrieved 7 May 2020
  4. "The Woman Who Started It All", Jamaica Gleaner, 13 October 2013. Retrieved 13 October 2013