lugha
sw Mtumiaji huyu ni mwongeaji wa Kiswahili Fasaha.


Naitwa Yona Fares Maro , Naishi na Kufanya kazi , Dar es salaam Tanzania , Nimesomea masuala ya Computer na Biashara lakini nimezamia zaidi kwenye masuala ya Computer haswa katika masuala ya Uchunguzi na Usalama wa computer na ufundi kidogo , nimekuwa katika sekta hii kwa zaidi ya miaka 3 mpaka sasa , kwa kufanya kazi na watu mbalimbali , kuwakilisha mada katika makongamano kwenye sehemu za makazi na vyuo mbali mbali Kwa Lugha ya kiswahili .

Kwa sasa naendelea kusomea zaidi masuala ya TEKINOLAHOMA katika chuo kikuu kimoja tawi la Nairobi Kenya , Napenda kuona wananchi popote walipo wanapata nafasi ambazo mimi nimezipata za kusoma na kufanya kazi kadhaa katika kuleta maendeleo katika jamii zao .