One Jerusalem, yaani Jerusalem Moja, ni shirika lenye dhamira ya "kudumisha Yerusalemu iliyounganika kama mji mkuu usiogawanyika kwa Israeli".

Ilianzishwa kama jibu kwa Mchakato wa Amani wa Oslo, haswa, kutokana na wasiwasi kuona kwamba suluhu hiyo inaweza kusababisha mamlaka ya Wapalestina juu ya Mlima wa Hekalu la Jerusalemu ili kuwa na amani.