Podikasiti ni neno lililoanza kutumiwa mwaka 2004 pale matumizi ya programu ya RSS ilipoanza kutumiwa kusambaza matangazo kwa ajili ya kusikiliza kupitia tarakilishi au zana nyingine za mkononi kama vile aipodi.

Podikasti ikichezwa kwenye simu, kupitia vipokea sauti.
Podikasti ikichezwa kwenye simu, kupitia vipokea sauti.

Podikasiti ni mafaili ya video au sauti ambayo yako kwenye mtandao wa tarakilishi kwa ajili ya yeyote yule anayetaka kutazama au kusikiliza. Wana podikasiti wanasambaza kazi zao kwenye tovuti au blogu zao kwa taratibu mbalimbali. Wako wanaoweka mafaili ambayo mtu yeyote anaweza kuyapakua bure au kwa kulipia, lakini kitu kinachofanya podikasiti kuwa tofauti na mafaili, kwa mfano, ya muziki ambayo unaweza kuyapakua na kusikiliza ni kwamba podikasiti inatumia teknolojia ambayo matangazo mapya yanaletwa kwako bila kukuhitahi wewe kwenda kwenye tovuti au blogu ya mwana podikasiti.

Redio nyingi kama vile BBC, NPR (Marekani), hivi sasa zinatuma matangazo yao kwa wasikilizaji kwa kwa kutumia teknolojia ya podikasiti.

Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.