Prerna Singh Bindra

mhifadhi wa wanyamapori na mwandishi kutoka India

Prerna Singh Bindra kutoka Gurgaon, India ni mmoja wa waandishi wa habari wa mazingira na waandishi wa kusafiri. [1] [2] [3] Pia ni mhadhiri katika Kituo cha Taifa cha Sayansi ya Biolojia na amepokea Tuzo ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya Carl Zeiss.

Prerna ana Shahada ya Uzamili katika Ustawi wa Wafanyakazi kutoka Chuo Kikuu cha Gujarat na pia amefanya masomo ya shahada ya kwanza katika Uchumi katika Chuo cha St. Xaviers (Ahmedabad).

Alianza kazi yake katika usimamizi akiwa Mshirika wa Utafiti katika Taasisi ya Usimamizi ya India, Ahmedabad. Baada ya kugundua kuwa wito wake wa kweli ulikuwa uandishi, alianza kuandika kwa Sanctuary Asia. Baadaye alifanya kazi kwenye magazeti ya kila siku kama The Asian Age, The Pioneer, The Times of India, na mengineyo. [4]

Marejeo

hariri
  1. "LC|n 2005212576". viaf.org.
  2. "Prerna Singh Bindra". Conservation India. Iliwekwa mnamo 12 Februari 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Meet Prerna Singh Bindra". sanctuaryasia.com. Iliwekwa mnamo 12 Februari 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. "Review: Rage of the River by Hridayesh Joshi". hindustantimes.com/. 23 Septemba 2016. Iliwekwa mnamo 12 Februari 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)