Roketi (Kiingereza rocket) ni chombo chenye umbo la bomba kinachopazwa angani kwa nguvu ya gesi inayotoka nje. Tofauti na injini ya jeti roketi hubeba fueli yote ndani yake kwa hiyo inafanya kazi pia katika ombwe pasipo na oksijeni au dutu nyingine inayohitajika kwa kuchoma fueli ndani ya injini yake.

Roketi aina ya Soyuz-U, huko Baikonur cosmodrome katika nchi ya Kazakistani.

Roketi hutumiwa kama silaha ya kijeshi, kama alama kiashiria katika hali ya dharura, fataki na kwa usafiri wa anga-nje.


Astrowiki.PNG
Mradi wa Astronomia Makala hii imewahi kukaguliwa na kuboreshwa kwenye warsha ya pamoja ya Jenga Wikipedia ya Kiswahili, Wikimedia Community User Group Tanzania na ASSAT. Imepewa hali ya ulinzi. Tunaomba mapendekezo yote ya usahihisho na nyongeza zipelekwe kwanza kwenye ukurasa wa majadiliano