Rosa Hilda Ramos ni mpokeaji wa pili kutoka Puerto Rico wa Tuzo ya Mazingira ya Goldman, tuzo ya kifahari inayotolewa kwa wanamazingira wa ngazi ya chini kutoka duniani kote na maarufu kama "Tuzo ya Nobel ya Kijani". Mama wa nyumbani na mwanaharakati wa mazingira aliyeishi katika mji wake wa Catano, Puerto Rico, Ramos alipokea tuzo kwa kusaidia kuokoa mikoko ya Las Cucharillas kutokana na maendeleo. Pia alifanikiwa kupambana na mchafuzi mkuu wa hewa wa eneo hilo— Mamlaka ya Nishati ya Umeme ya Puerto Rico (PREPA) inayomilikiwa na serikali-- na kulazimisha shirika la umma kupunguza kwa kiasi kikubwa kipigo cha uchafuzi wa mazingira unaotolewa angani na kulazimisha kulipa faini ya shirikisho ya dola milioni 7.

Tuzo ya Mazingira ya Goldman ya 2008, ambayo inajumuisha ruzuku ya fedha ya $150,000, ilitolewa kwa wapokeaji saba huko San Francisco, California mnamo Aprili 14, 2008.