Selemon Barega Shirtaga (alizaliwa 20 Januari 2000) ni mkimbiaji wa umbali mrefu wa Ethiopia ambaye anashindana hasa katika mita 5,000 na mita 10,000.

Selemon kwenye Mashindano ya Dunia ya U20 ya 2016 huko Bydgoszcz
Selemon kwenye Mashindano ya Dunia ya U20 ya 2016 huko Bydgoszcz

Alishinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 10,000 katika michezo ya Olimpiki ya majira ya joto ya Tokyo 2020. Aliiwakilisha nchi yake katika mashindano ya dunia ya mwaka 2017 akimaliza wa tano katika fainali. Pia alishinda medali za dhahabu katika Mashindano ya Dunia ya U20 ya 2016 na Mashindano ya Dunia ya U18 ya 2017. Alishinda medali ya fedha katika mbio za mita 5000 katika mashindano ya riadha ya dunia ya mwaka 2019 mjini Doha, Qatar.

Marejeo hariri