Kwa mwelekeo wa kidini tazama Sufii, Usufii

Sufi (kar. صوف suf[1]) ni jina kwa nyuzi laini kama pamba zinazotoka kwenye matunda ya msufi (miti ya jenasi Bombax, Ceiba na Rhodognaphalon).

Sufi katika tunda la msufi mweupe, Ceiba pentandra, kisiwani Unguja
Msufi-pori (Rhodognaphalon schumannianum)

Sufi hutumiwa kwa kujaza magodoro, kama kalafati kuziba nyufa kati ya mbao za mashua n.k. Haifai kwa kutengeneza nyuzi ndefu na vitambaa.

Mara nyingi neno hili linatumiwa pia kwa kutaja sufu yaani manyoya ya kondoo.

Marejeo hariri

  1. neno asilia katika Kiarabu صوف suf lamaanisha nywele manyoya laini ya kondoo na wanyama wengine limeingia katika Kiswahili kwa maumbo ya sufi na sufu