Tarbia ndiyo aina ya shairi rahisi sana kuandika na waandishi wengi hutumia aina hiyo ya shairi.

Ni shairi lenye mishororo minne katika kila ubeti na vipande viwili katika kila mshororo.

Vipande hivyo hujulikana kama Ukwapi na utao.

Mfano wa mashairi ya tarbia:

Kalamu yangu kichwani, ninacho cha kuandika

Kilichopo akilini, kwa wengi kitasikika

Kwa mtu nilo makini, kwake haya yatafika

Tungeheshimu kalamu, ingelindika sheria.

Makala hii kuhusu mambo ya fasihi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tarbia kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.