Tesla, Inc ni kampuni ya teknolojia ya Marekani inayojulikana zaidi kwa kuzalisha magari ya umeme na teknolojia ya uhifadhi wa nishati. Ilianzishwa mnamo mwaka 2003 na mjasiriamali Elon Musk na wengine, na imekuwa ikiongoza katika mapinduzi ya magari ya umeme. Tesla pia inajihusisha na uzalishaji wa betri za lithiamu-ion kwa matumizi ya gari, pamoja na kutoa suluhisho za uhifadhi wa nishati kwa matumizi ya nyumbani na biashara[1].

Tesla Motors logo

Tesla, Inc nimashuhuri kwa mifano kama vile Tesla Model S, Model 3, Model X, na Model Y, Tesla imekuwa ikiendeleza teknolojia mpya ya usafiri inayohusisha uwezo wa kuendesha gari kwa kutumia mfumo wa kujitegemea wa Tesla, unaojulikana kama Autopilot. Kampuni hiyo pia ina miradi kadhaa inayohusiana na nishati mbadala, kama vile jua na nishati ya upepo.

Tesla imekuwa mojawapo ya kampuni inayoongoza duniani katika sekta ya magari ya umeme na imekuwa ikichangia kwa kiasi kikubwa katika kusukuma mbele mabadiliko ya usafiri endelevu.

Tanbihi hariri

  1. "Tesla: A Carmaker With Silicon Valley Spark", Bloomberg.com, July 30, 2007. (en) 
  Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.