Bahari ya Kaspi

(Elekezwa kutoka Bahari Kaspi)

Bahari ya Kaspi (Kiarabu: بحر قزوين Baḥr Qazvin; Kiajemi: دريا خزر darya khazar; Kirusi: Каспийское море kaspiiskoye more) ni ziwa kubwa kabisa duniani lenye eneo la km² 371,000 na mjao wa km³ 78,200. Liko kati ya Azerbaijan, Urusi, Kazakhstan, Turkmenistan na Uajemi.

Bahari ya Kaspi kutoka angani.
Stenka Razin (Vasily Surikov)

Kimo chake kinafikia mita 1,025.

Huitwa "bahari" kwa sababu maji yake ni ya chumvi ingawa si kali sana kama ya bahari yenyewe.

Maji ya chumvi hariri

Upande wa kaskazini inaingia mito miwili mikubwa ya Volga na Ural. Inasababisha kiasi kidogo cha chumvi upande huo wa kaskazini. Asilimia ya chumvi huonegezeka kuelekea kusini.

Madini hariri

Chini ya bahari kuna akiba kubwa za mafuta ya petroli na gesi, hasa karibu na Baku. Katika hori ya Kara-Bogas chumvi hulimwa.

Viungo vya Nje hariri