Bangkok ni mji mkuu na pia mji mkubwa wa Uthai katika Asia Kusini-Magharibi. Kuna wakazi milioni saba walioandikishwa lakini imekadiriwa ya kwamba jumla ya wakazi inafikia hadi milioni 14-15.

Jiji la Bangkok
Nchi Uthai
Hekalu ya Wat Phra Kaew mjini Bangkok

Mji uko kwa 13°45′N 100°31′E kando la mto Chao Phraya karibu na mdomo wake katika Ghuba la Uthai.

Mji ulianzishwa kama bandari kwa ajili ya mji mkuu wa kale Ayutthaya. Mfalme Rama I aliyeanzisha utawala wa familia ya kifalme ya Chakkri alijenga jumba lake hapo mtoni na kuanzisha mji mkuu mahala pa leo.

Kuna mahekalu 400 ya Ubuddha mjini hasa Wat Phra Kaew.

Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bangkok kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu: