Chama tawala ni istilahi ya siasa inayotaja chama kilichoshika uongozi wa nchi, kwa kawaida kupitia uchaguzi.

Shida inayoweza kujitokeza ni kudai chama hicho kiendelee kutawala milele, hata bila ridhaa ya wananchi.

Wanaopinga uongozi wa chama tawala na serikali yake wanaitwa wanasiasa wa upinzani.