Chuo Kikuu cha Babcock

Chuo Kikuu cha Babcock ni chuo kikuu cha binafsi cha Kikristo, Nigeria inayomilikiwa na kuendeshwa na Kanisa la Waadventista Wasabato nchini Nigeria. Chuo kikuu kina umbali sawa kutoka Ibadan na Lagos.

Chuo Kikuu cha Babcock
WitoKnowledge, Truth, Service
Kimeanzishwa1959
AinaPrivate
Makamu wa chanselaJ Kayode Makinde
ChaplainDr. Israel B. Olaore
Wanafunzi6.000
MahaliIkeja, Lagos, Nigeria
Former namesAdventist College of West Africa, Adventist Seminary of West Africa
Government Accreditation1999
Tovutiwww.babcockuni.edu.ng

Uandikishaji ulikuwa 6,000 mwaka wa 2009. [1]

Historia hariri

Chuo Kikuu cha Babcock kilipewa jina la Marekani aitwaye Daudi C. Babcock, ambaye alianzisha kazi cha Waadventista Wasabato nchini Nigeria mwaka 1914. Alikuwa mjini Erunmu katika Oyo, Nigeia.

Chuo hiki kikuu kilianzishwa kama Chuo cha Waadventista Afrika Magharibi mwaka 1959, kikiwa na wanafunzi 7. Mwaka wa 1975, kilibadilishwa jina lake na kuwa Seminari ya Wasabato Afrika Magharibi. Chuo hiki kikuukilizinduliwa rasmi tarehe 20 Aprili 1999. [2]

Maeneo ya elimu hariri

Mipango ya kielimu katika Chuo Kikuu cha Babcock imeundwa katika shule nne na idara mbalimbali ambayo ni ya msingi ambapo mipango ya kufundisha, kujifunza na utafiti huundiwa. Kuna pia mipango ya kuanziha shule ya matibabu ambayo inaweza kuitwa Shule ya Utabibu ya Ben Carson. Sasa hivi Shule hii inaendesha shughuli za kutafuta fedha ili kukamilisha mradi wa Naira bilioni 3 [3] Nazo ni:

  • Kitivo cha Elimu & Utu
    • Idara ya Elimu na Mafunzo ya Kawaida
    • Idara ya Historia na Mafunzo ya kitaifa
    • Idara ya Lugha na fasihi
    • Idara ya Kuwasiliana kwa umma
    • Idara ya mafunzo ya dini
  • Shule ya Sayansi ya Sheria na Usalama
    • Idara ya Kimataifa ya Sheria
  • Shule ya Usimamizi na Sayansi Sociaya Kijamiil Sciences
    • Idara ya Akaunti
    • Idara ya Usimamizi wa Biashara na soko
    • Idara ya Uchumi, Benki na Fedha
    • Idara ya Sayansi ya Siasa na Usimamizi wa Umma
  • Shule ya Sayansi na Teknolojia
    • Idara ya Kilimo
    • Idara ya Msingi na Sayansi
    • Idara ya Sayansi ya Kompyuta na Hisabati
    • Idara ya Sayansi ya Afya

Marejeo hariri

  1. Chuo kikuu cha Nigeria cha Wasabato kilipongezwa kwa viwango vya elimu. Adventist News Network. Ilipakuliwa 2009-03-22.
  2. Historia. Archived 24 Desemba 2008 at the Wayback Machine. Babcock University. Ilipakuliwa 2009-03-22.
  3. Academics. Archived 5 Oktoba 2011 at the Wayback Machine. Babcock University. Ilipakuliwa 2009-03-22.

Viungo vya nje hariri