Chuo Kikuu cha Botho

Chuo Kikuu cha Botho ni mtoa elimu wa juu binafsi mkubwa zaidi nchini Botswana, kilianzishwa mwaka 1997. Chuo hiki kinatoa astashahada, stashahada na shahada ya awali katika uhasibu na sayansi ya kompyuta. Ni taasisi ya kwanza ya elimu ya juu binafsi nchini kupata uidhinisho kutoka Baraza la Elimu ya Juu (kwa kiingereza: Tertiary Education Council - TEC). Programu zake zote pia zinathibitishwa na Mamlaka ya Kudhibiti kiwango cha Elimu ya Botswana. Chuo hiki kimefundisha wahitimu 16,000 na kina wanafunzi 4,000, wakisaidiwa na wafanyakazi 150 wa kitaaluma.[1]

Programu za Botho za Sayansi ya Kompyuta zimeshirikiana na taasisi za kimataifa kama vile NIIT, Chuo Kikuu Huria na Chuo Kikuu cha Teesside.[2]

Marejeo

hariri
  1. "Welcome to Botho University". web.archive.org. 2013-08-03. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2013-08-03. Iliwekwa mnamo 2024-07-16.{{cite web}}: CS1 maint: bot: original URL status unknown (link)
  2. BizTechAfrica Editorial Team (2016-09-21). "2016 Linkz ICT challenge concluded". Biztech (kwa American English). Iliwekwa mnamo 2024-07-16.