Filipo II wa Masedonia

(Elekezwa kutoka Filipo II wa Makedonia)

Filipo II wa Masedonia[1] (kwa Kigiriki: Φίλιππος Β΄ ὁ Μακεδών, Phílippos II ho Makedṓn; 382 KK336 KK) alikuwa mfalme wa Masedonia katika Ugiriki wa Kale kuanzia mwaka 359 KK hadi alipouawa.

Sanamu ya Filipo II.

Mnamo 500 KK kulikuwako ufalme ulioitwa Masedonia ambao ulihesabiwa kama sehemu ya utamaduni wa Ugiriki wa kale na wafalme waliruhusiwa kwenye michezo ya Olimpiki ya madola ya Wagiriki.

Pamoja na sehemu nyingi za Ugiriki ufalme huo ulipaswa kukubali ubwana wa Milki ya Uajemi, lakini Filipo alifaulu kuurudisha uhuru akaendelea kuifanya Masedonia kuwa dola kiongozi kati ya madola madogo ya Ugiriki.

Mwanawe Aleksanda Mkuu aliimarisha utawala wake juu ya Wagiriki wengine na kushambulia Milki ya Uajemi na hatimaye kuivamia na kuishinda kwa jeshi kutoka sehemu zote za Ugiriki.

Tanbihi hariri

  1. Philip II of Macedonia: Ian Worthington, Yale University Press, ISBN 0300164769, 9780300164763

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Filipo II wa Masedonia kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.