Fly540

ni kampuni ya ndege inayosafirisha kwa gharama nafuu mjini Nairobi

Fly540 (kwa Kiingereza: Five Forty Aviation Ltd.) ni kampuni ya ndege inayosafirisha kwa gharama nafuu mjini Nairobi, Kenya. Husafirisha abiria na mizigo, nchini na pia kitaifa[1].

Fly540
Faili:Optimized image b9d4dbdd.png
IATA
5H
ICAO
FFV
Callsign
SWIFT TANGO
Kimeanzishwa 2006
Vituo vikuu Jomo Kenyatta International Airport
Ndege zake 5
Shabaha 14
Nembo Simplifly
Makao makuu Nairobi, Kenya
Watu wakuu Neil Steffen, Don Smith (Chief Exectutive Officer)
Tovuti http://www.fly540.com/

Historia hariri

Kampuni hii ya usafiri wa ndege ilianza shughuli kati ya Nairobi na Mombasa tarehe 24 Novemba 2006. Awali ilisafiri mara mbili kwa siku kwa kutumia ndege ya ATR 42 yenye viti 48[2]. Jina la kampuni linahusu bei yake ya nauli ambayo ni Sh 5,540 kwa watu wazima pamoja na nauli ya kurudi, kusafiri kati ya miji iliyotajwa hapo juu [3].

Lonrho Afrika ni mwekezaji mkubwa katika kampuni, ambapo ililipa dola milioni 1.5 ili kumiliki asilimia 49 za hisa.

Mwezi Mei mwaka wa 2007 kampuni ilileta ndege mbili aina ya Bombardier Dash 8 Q100 ili kuongeza idadi ya wasafiri, na kuiruhusu kuendeleza njia mpya za usafiri wa ndani. Idadi ya abiria iliongezeka kwa asilimia 93 hadi 171,160 mwaka uliOmalizika 30 Septemba 2008, kutoka 88,571 mwaka wa 2007. Wakati huohuo, kipengele cha mzigo kilifikia asilimia 63, kutoka asilimia 65,8 mwaka wa 2007[4].

Miradi ya Afrika hariri

 
Ndege aina ya ATR 42 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe

Mpango wa awali wa usafiri wa ndege ulikuwa - isipokuwa usafiri wa mizigo - mpango wa usafiri wa abiria kati ya Nairobi na Mombasa, na Kisumu ikawa shabaha mnamo Januari mwaka wa 2007[3]. Usafiri wa kila siku kati ya Nairobi na Malindi uliongezwa katika idadi ya huduma mwezi wa Februari mwaka wa 2007[5].

Oparesheni za kimataifa Zilianzia katika Oktoba mwaka wa 2007 kwa kusafiri kati ya Juba katika Sudan Kusini na Goma katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo [6]. Entebbe iliongezwa katika Februari mwaka wa 2008. Kiwanda cha Nairobi kina mipango ya kuendelea upanuzi hadi Rwanda, Msumbiji na Burundi mwaka 2009 [7] Lengo la Kampuni ni kuwa msafiri wa Afrika, kupitia upanuzi na nyongeza mbili za viwanda:

"... Tutafungua kituo Kigali na kisha twende Afrika Magharibi. Ghana itakuwa kiwanda cha Afrika Magharibi. Katika Kusini mwa Afrika, tutakuwa na kiwanda Angola, hivyo itakuwa kampuni ya usafiri wa ndege Afrika kwa gharama nafuu [8]

Ilipokea ruhusa kuanza oparesheni nchini Angola mwezi Aprili 2009. Mipango ya kwanza ni usafiri wa ndani hadi Cabinda, Luanda, Soyo, Benguela, Huambo na Malanje [9] lakini katika kanda upanuzi utafanyika haraka kama soko la ndani litaonyesha mafanikio yake [10] Mwezi Juni 2009, iliripotiwa kuwa Fly540 ilikuwa ikitayarisha kuanzisha kiwanda nchini Zimbabwe [11]

Shabaha hariri

Kufikia Juni 2009, Fly540 ilikuwa na shabaha zifuatazo:

  • Kenya
    • Eldoret (Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Eldoret)
    • Kisumu (Uwanja Wa Ndege wa Kisumu)
    • Kitale (Uwanja Wa Ndege wa Kitale )
    • Lamu (Uwanja Wa Ndege wa Manda)
    • Lodwar (Uwanja Wa Ndege wa Lodwar)
    • Malindi (Uwanja Wa Ndege wa Malindi)
    • Masai Mara (Uwanja Wa Ndege wa Mara Serena )
    • Mombasa (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Moi)
    • Nairobi (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta)
  • Sudan
    • Juba (Uwanja Wa Ndege wa Juba)
    • Rumbek (Uwanja Wa Ndege wa Rumbek)
  • Tanzania
    • Kilimanjaro (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro
    • Zanzibar (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar)
  • Uganda
    • Entebbe (Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe)

Ndege hariri

Fly540 ina ndege zifuatazo (kufikia Januari 2009):

Katika Januari 2008, kampuni hii ilitia saini dola million 150 za Amerika kwa mkataba wa ATR nane hadi 72-500skupokezwa mwaka wa 2008 na 2009.[12].

Ajali na matukio hariri

Tarehe 13 Agosti 2008, ndege aina ya Fokker F27-500 ilipania karibu na Uwanja wa Ndege wa Namber Konton Mogadishu, Somalia. Wafanyikazi wa ndege wote watatu walikufa. Ndege ilisemekana ilikuwa ikisafirisha miraa.[13] Ndege kuondoka kutoka Uwanja Wa Ndegewa Wilson mjini Nairobi. Nambari yake ya usajili ni 5Y BVF [14]

Viungo vya nje hariri

Marejeo hariri

  1. "Directory: World Airlines", Flight International, 2007-04-03, p. 83. 
  2. Airliner World Januari 2007
  3. 3.0 3.1 The Standard, 18 Januari 2007: Tai mpya angani
  4. Lonrho PLC, 30 Machi 2009: Taarifa ya Mwaka 2008 Archived 4 Juni 2009 at the Wayback Machine.
  5. Fly540 habari
  6. The Standard, 26 Septemba 2007: Fly540 yalenga Sudan na DRC
  7. Lonrho PLC, 11 Novemba 2008: Lonrho yafufua £ milioni 15.6 Kuendeleza Biashara Archived 24 Februari 2012 at the Wayback Machine.
  8. The Monitor, 12 Agosti 2008: Afrika: Fly540 yalenga bara
  9. Lonrho PLC, 29 Aprili 2009: Air Services Licence Imetolewa kwa Fly540 Angola Archived 17 Februari 2012 at the Wayback Machine.
  10. Lonrho PLC, 11 Novemba 2008: Lonrho huwafufua £ milioni 15.6 Kuendeleza Biashara Archived 24 Februari 2012 at the Wayback Machine.
  11. Zimabwe Independent, 4 Juni 2009: Zimbabwe: LonZim yapanga kuanzisha kampuni ya usafiri wa Ndege
  12. EADS, 11 Januari 2008: Lonrho kupata 8 ATR 72-500s kwa ndege Fly540
  13. www.bloomberg.com - Kenyan Cargo Plane yapania karibu na mji mkuu wa Somalia; Watatu wauawa
  14. Daily Nation, 13 Agosti 2008: ndege yapania mjini Mogadishu Archived 24 Desemba 2018 at the Wayback Machine.