Gervas Kasiga

Muigizaji na mtayarishaji filamu wa Tanzania

Gervas A. Kasiga (anafahamika zaidi kama Chuma au Junior.[1]; alizaliwa 4 Februari 1982) ni mwigizaji wa filamu, mwandishi wa miswada ya filamu, mshairi, mwongozaji wa filamu na mhadhiri wa chuo kikuu kutoka nchini Tanzania.[2][3]

Gervas Kasiga
Gervas Kasiga
AmezaliwaGervas 'Rutakirwa' Kasiga
UtaifaMTanzania
MhitimuB.A Fine and Performing Arts & M.A Kiswahili Literature, PhD in Kiswahili
Kazi yakeMwigizaji, Mwandishi wa Miswada ya Filamu, Mwongozaji wa Filamu, Mhadhiri wa Filamu na Fasihi
Miaka ya kazi1999-hadi sasa

Anafahamika sana kwa kuongoza filamu maarufu ya "Fake Pastors (2007)" na kuongoza kuchagua waigizaji wa filamu ya Bongoland II.

Ameandika miswada kadhaa ya Michezo ya Kuigiza ya Runinga (Tamthilia) kama vile "Gharika" na "Dira", miswada ya filamu maarufu za Unfortunate Love, Ripple of Tears, Village Pastor, Wende na nyinginezo.

Mwaka 2011 filamu yake fupi ya Wende ilichaguliwa kuoneshwa katika Tamasha la Sita la Filamu la Kimataifa la Kenya (KIFF). Vilevile amepata kuwa balozi wa Tamasha la Filamu la Kimataifa la Zanzibar (ZIFF) akiwakilisha wanafilamu wa ki-Tanzania.

Kasiga ameshafanya kazi mbalimbali za kisanaa na mashirika kama AMREF, PATHFINDER, THE NATURE AND CONSERVANCY, The International Theatre and Literacy Project (ITLP), CRDB - TANZANIA, College of Mathematics and Natural Science - University of Dodoma, Vocation Training Centre of Tanzania (VETA), Regina University - Canada na mengine mengi.[4] Ameshaendesha mafunzo mbalimbali ya uigizaji, uandishi wa miswada ya filamu, uchukuaji picha za video pamoja uongozaji katika mikoa ya Mwanza, Kigoma, Dodoma na Dar es salaam. Mafunzo hayo amekuwa akiyafanya aidha kupitia taasisi yake ya Dodoma Arts Center (DAC) au kupitia kampuni yake ya Bona Fide Films ama kwa kushirikiana na mashirika ya ndani na ya kimataifa.

Msanii huyu pia ni Mhadhiri wa masomo ya Fasihi na Filamu kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma - Tanzania.

Vilevile ni mwanablogu, anaendesha blogu ya Sebuleni. Gervas Kasiga katika seti ya Bongoland II[5][6]

Maisha ya awali hariri

Filmografia hariri

Na. Jina Mwaka Maelezo
1 Radi 2003 Tamthiliya—Mwigizaji (imetayarishwa na ITV).
2 Jahazi 2003 Tamthiliya—Mwigizaji (imetayarishwa na ITV).
3 Dira 2004 Tamthiliya—Mwigizaji & Mwandishi Muswada (imetayarishwa na ITV).
4 Sayari 2004 Tamthiliya—Mwigizaji (imetayarishwa na ITV).
5 Falcon Death 2005 Mwongozaji msaidizi. Imetayarishwa na Profesa Daniel kutoka Chuo Kikuu West Virginia.
6 Gharika 2005 Tamthiliya—Mwigizaji & Mwandishi Muswada (imetayarishwa na ITV).
7 Fake Pastors 2007 Mwandishi Muswada & Mwongozaji
8 Unfortunate Love 2008 Mwandishi Muswada
9 Igizo la Uchaguzi 2010 Imetayarishwa na Kuongozwa na hayati Edwin Semzaba
10 Wende 2011 Filamu fupi (Matayarishaji na Mwongozaji).
11 Distress in Zanzibar 2013 Mwandishi na Mwongozaji
12 Jukwaa Langu 2015 Mfululizo wa mahojiano kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2015
13 Soma Sasa 2016 Mpiga Picha Jongevu na Mwongozaji
14 Marita 2017 Filamu fupi (Matayarishaji na Mwongozaji).
15 Tuungane Drama Training Session 2017 Mwongozaji
16 Simulizi za Mjomba 2019 Mwandishi Muswada

Mashairi hariri

Na. Jina Mwaka Maelezo
1 Mama Afrika 2021 Pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan
2 Pambazuko Toshelevu 2021 Kumbukizi ya hayati John Magufuli

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  1. Majina hayo aliyapata kupitia mifululizo ya vipindi maarufu vya tamthilia za kituo cha runinga cha ITV (Tanzania) kupitia kundi la Kaole Sanaa Group.
  2. "Gervas Kasiga | The University of Dodoma, Tanzania - Academia.edu". udom.academia.edu. Iliwekwa mnamo 2022-07-01. 
  3. "Gervas Kasiga - Lecturer - University Of Dodoma | Business Profile". Apollo.io. Iliwekwa mnamo 2022-07-01. 
  4. "Kasiga". 2008-08-01. 
  5. Kibira anamtambulisha Kasiga katika ushiriki wa Bongoland II 2008 - Kibira blogu.
  6. Gervas Kasiga katika blogu ya Sebuleni.