Hifadhi ya Taifa ya Arusha yenye Mlima Meru, wenye volkano maarufu na mwinuko wa m. 4566 (futi 14990), inapatikana katika Mkoa wa Arusha, Kaskazini Mashariki mwa Tanzania, umbali wa kilometa 32 kutoka mji wa kitalii wa Arusha.

Chui katika mawindo
Flamingo wa hifadhi ya Arusha

Maeneo muhimu ya hifadhi hariri

Hifadhi hiyo ni ndogo (ina ukubwa wa kilometa za mraba 542 tu) lakini ina mandhari yenye maeneo matatu tofauti.

1. Katika magharibi, kreta ya mlima Meru inafanya Mto wa Jekukumia, kilele cha Mlima Meru kwa juu ni cha mviringo. Unafanya hifadhi kuwa na mazingira ya baridi.

2. Kreta ya Ngurdoto Kusini-Mashariki ni yenye uoto wa nyasi.

3. Maziwa yenye kina, Mamaella Kaskazini-Mashariki yana rangi tofauti za algali na hujulikana kwa kuwa na ndege wenye midomo mirefu wanaoishi pembezoni mwa maziwa (sehemu zenye matope).

Viumbe hai hariri

Hifadhi hii ni maarufu kwa wanyama jamii ya tumbili wajulikanao kama mbega weusi na weupe.

Wanyama wengine wanaopatikana kwa wingi katika hifadhi hii ni pamoja na twiga, pundamilia, nyati na digidigi.

Aidha unaweza kuwaona chui wakibarizi katika vivuli vya matawi ya miti inayokingwa na maanguko ya maji huku makundi kadhaa ya batamaji yakitafuta wadudu katika maziwa ya Momella.

Zaidi ya aina 400 za ndege wamethibitika kupatikana ndani ya hifadhi hii.

Mambo yanayoweza kufanyika ndani ya hifadhi hii hariri

Safari ya miguu kupanda mlima Meru ni moja ya burudani muhimu katika hifadhi hii: mpandaji anahitaji siku 3-4 kupanda mlima.

Wakati mzuri wa kutembelea hifadhi hii ni kati ya mwezi Juni na Februari ingawa mvua inaweza kunyesha mwezi Novemba.

Picha hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

Majarida ya hifadhi za Taifa Tanzania

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Arusha bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hifadhi ya Arusha kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.