Maandishi madogo

Ugawaji wa karatasi ya ukubwa A0 hadi A9

ISO 216 ni orodha ya vipimo sanifu iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Usanifishaji (ISO) kwa ajili ya fomati za karatasi. Orodha hii inafafanua fomati za karatasi za aina "A" na "B" pamoja na A4 ambayo ni ukubwa unaotumiwa zaidi duniani. Zinatumiwa kote duniani isipokuwa Marekani bado wanatumia fomati tofauti.

Fomati zote za ISO 216 (na vipimo vya kuambatana nayo ISO 217 na ISO 269) vinafuata uhusiano wa 1: kati ya upande mrefu na upande mfupi. Faida yake ni ukikunja karatasi hizi kwa nusu yake, hata sehemu hizi zitakuwa tena na uhusiano huohuo baina ya upande ndefu na fupi. Pia eneo la kila fomati ni nusu ya eneo la fomati kubwa zaidi.

Fomati ya kimataifa ya ISO 216 inafuata utaratibu uliofafanuliwa nchini Ujerumani tangu mwaka 1922 kwa jina la DIN 476.

Vipimo vya karatasi za fomati za A na B chini ya ISO 216 na C chini ya ISO 269 hariri

Fomati za karatasi za ISO 216
(mm × mm)
Fomati za A Fomati za B Fomati za C
A0 841 × 1189 B0 1000 × 1414 C0 917 × 1297
A1 594 × 841 B1 707 × 1000 C1 648 × 917
A2 420 × 594 B2 500 × 707 C2 458 × 648
A3 297 × 420 B3 353 × 500 C3 324 × 458
A4 210 × 297 B4 250 × 353 C4 229 × 324
A5 148 × 210 B5 176 × 250 C5 162 × 229
A6 105 × 148 B6 125 × 176 C6 114 × 162
A7 74 × 105 B7 88 × 125 C7 81 × 114
A8 52 × 74 B8 62 × 88 C8 57 × 81
A9 37 × 52 B9 44 × 62 C9 40 × 57
A10 26 × 37 B10 31 × 44 C10 28 × 40

Marejeo hariri

Viungo vya Nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: