Jemimah Kariuki ni daktari wa Kenya aliyebobea kwenye maswala ya afya ya uzazi na mtoto na dawa. Wakati wa janga la Ugonjwa wa Virusi vya Korona 2019 alipanga huduma ya gari la wagonjwa ambayo iliwawezesha wajawazito kupata huduma ya uzazi. Aliorodheshwa kama mmoja wa BBC's 100 Women mnamo mwaka 2020.

Kazi hariri

Kariuki ni mkazi na ni daktari wa magonjwa ya uzazi na kizazi katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Yeye ndiye mwanzilishi wa Klabu ya Amani, iliyoanzishwa kutokana na ghasia za baada ya uchaguzi mwaka wa 2007, na Klabu ya Afya ya Umma, ambayo imejitolea katika kuzuia na kuhamasisha kuhusu saratani ya shingo ya kizazi. Wakati wa janga la COVID19 nchini Kenya, kama daktari wa uzazi, aliona kupungua kwa kasi kwa wagonjwa wa uzazi, lakini ongezeko la matatizo, hasa wakati wa saa za kutotoka nje.[3][4] Kenya ni mojawapo ya nchi zilizo na viwango vya juu zaidi vya vifo vya akina mama na watoto, jambo ambalo amri ya kutotoka nje ilisababisha kuongezeka, kulingana na wataalam. Kariuki aligundua kwamba upatikanaji wa huduma za afya ulicheleweshwa kwa sababu ya uhaba wa usafiri. Hapo awali alitumia mtandao wa kijamii wa Twitter kuomba usaidizi kutoka kwa mashirika ya serikali na makampuni ya kibinafsi kuwasafirisha wazazi wajawazito hadi hospitalini. Wazo hili lilisababisha, huduma ya bure ya ambulensi.

Tuzo hariri

Tarehe 23 Novemba 2020, Kariuki alikuwa kwenye orodha ya BBC ya wanawake 100 wenye ushawishi mkubwa zaidi wa mwaka.

Mei 25, 2021 - Tuzo la Mkurugenzi Mkuu wa WHO kwa Afya Ulimwenguni 2021 kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza afya duniani.

  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jemimah Kariuki kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.