Kamusi Sanifu ya Kompyuta

(Elekezwa kutoka Kamusi ya Kompyuta)

Kamusi Sanifu ya Kompyuta (kifupi: KSK) ni kamusi ya Kiswahili iliyotolewa mwaka 2011 na Taasisi ya Taaluma za Kiswahili ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Ilitungwa na Omari M. Kiputiputi kwa kushirikiana na mratibu Selemani S. Sewangi.

Maelezo yote ya msamiati ni kwa lugha ya Kiswahili kwenye kurasa zaidi ya 600.

Kamusi hii haina sehemu ya Kiingereza-Kiswahili.

Marejeo hariri

  • Omari Kiputiputi: KAMUSI SANIFU YA KOMPYUTA, Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Toleo la Kwanza 2011, ISBN 9789987531127
  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kamusi Sanifu ya Kompyuta kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.