Khalid Aucho (amezaliwa Jinja, 8 Agosti 1993) ni mchezaji wa soka wa kitaalamu kutoka Uganda. Anacheza kama kiungo wa kati wa ulinzi katika klabu ya Young Africans nchini Tanzania na timu ya taifa ya Uganda, Uganda Cranes12.

Picha ya Khalid Aucho

Historia yake

hariri

Khalid Aucho alisoma katika shule za Namagabi Primary School, St Thudus (O-level), na Iganga Mixed School (A-level).

Kazi yake katika klabu

hariri

Alicheza katika klabu ya Gor Mahia F.C. nchini Kenya kutoka mwaka 2015 hadi Mei mwaka 2016. Baadaye, alijiunga na klabu ya Baroka nchini Afrika Kusini. Mwaka 2021, alijiunga na klabu ya Young Africans nchini Tanzania[1].

Mafanikio

hariri

Khalid Aucho aliteuliwa kuwa Mchezaji Bora wa Msimu wa Uganda na 256 FOTY Award mwaka 2023. Pia, klabu yake ya Young Africans imekuwa ikifanya vizuri na imemteua kwenye orodha ya wachezaji bora wa mwezi Novemba mwaka 2023.

Mafanikio ya kimataifa

hariri

Alisaidia timu ya Uganda kufuzu katika Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) kwa mara ya kwanza baada ya miaka 38 mnamo Septemba 2016. Kwa sasa, Khalid Aucho anaendelea kufanya vizuri katika soka na anachangia katika mafanikio ya timu yake ya Young Africans.

Tanbihi

hariri
  Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Khalid Aucho kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.