Kichin ya Khumi (au Kikhumi) ni lugha ya Kisino-Tibeti nchini Bangladesh, Uhindi na Myanmar inayozungumzwa na Wachin. Mwaka wa 2006 idadi ya wasemaji wa Kichin ya Khumi nchini Myanmar imehesabiwa kuwa watu 60,000. Pia kuna wasemaji 2090 nchini Bangladesh (2005). Idadi ya wasemaji nchini Uhindi haijulikani. Kufuatana na uainishaji wa lugha, Kichin ya Khumi iko katika kundi la Kisal.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kichin-Khumi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.